Wednesday, December 31, 2014

Nakushukuru Mungu kwa yote uliyonitendea kwa mwaka 2014


Shukrani kwa  Mungu kwa yote uliyonitendea mwaka 2014. Wapenzi wa Banzi wa Moro, mwaka huu nimeweza kufikisha posts 955, posts 353 zaidi ya mwaka jana (602). Nakushukuru sana Bw.Bello kwa changamoto yako wakati ule nilipokuwa niliponing'iniza posts 16 kwa mwaka, miaka miwili mfululizo!

Mafanikio haya yamepatikana kutokana na kuwa na vitendea kazi bora vya IT,safari za kikazi mikoani, shughuli za kanisa na familia pia. Wasomaji wa Blog hii wamekuwa wakinitia moyo sana kwa kuandika comments zao na wengine kunipigia simu baadhi yao ni Bi. Sophia Kizito, Bw. Charles John Arbogasty wa Botswana, Dada Appia Mkoba wa Norway, Dada Eddy Daulinge wa COSTECH aliyetoa maoni ya kutengeneza pesa kupitia blog hii (Nakungoja Sister), Dogo Fredy Mloka wa TTCL, Dr. Doreen Mloka wa Muhimbili University,Sister Ceasar Mloka a.k.a 'Mzungu'  mjisiriamali, Sister Slyvia Daulinge na mumewe Gaitan ambao walikuwa wananipa ujumbe-tumeona vitu vyako! Dada Meab, Dogo Frank Mdimi, Dogo Sily Jakka wa Dadaz Dar (a.k.a. Paroko), Bw.Philemon Kabandwa wa MAFC,Dadaz Ishika na Vidah wa DRD, Dr. Louis Kasuga wa ARI-Naliendele, Bw. Andrew Rabson Kwayu na vijana wake wa IT pale MAFC na wengine wengi.Asanteni sana.

Mategemeo yangu kwa mwakani ni kuboresha zaidi blog hii ili ipendeze na kuvutia wasomaji wengi na pengine kuifanya ya kibashara (kama itawezekana). Yeyote mwenye wazo la kuiboresha namkaribisha. NAWATAKIA MWAKA MPYA WENYE BARAKA ZA MUNGU.

Matombo Msalabani

Ukifika hapa, kushoto ni barabara inayoelekea makao makuu ya tarafa ya Matombo ambako ni Mtamba, barabara hiyo inakufikisha  hadi Kisaki ambako unaweza kupanda gari moshi kwenda Zambia au Dar Es Salaam! Kulia ni baraba kuelekea Matombo Mission, Tawa, Kibungo Juu,  Kibogwa, Nyachiro, Lusangalala, Konde,Mlono,Lanzi,Lukenge, na Kitungwa.

Kwenye bango la Matombo Secondary sijafurahishwa na jinsi Mission yao ilivyoandikwa- 'Always Forward.' Kwa kweli haileti maana hata kidogo.Tutashauriana na uongozi wa shule ili kuiboresha.

Tunauvuka mto Ruvu x 2



Tunaposafiri kutoka Dar kwenda Matombo lazima tuvuke mto wa Ruvu mara mbili. Hapa ni daraja la mto Ruvu unapokaribia Matombo. Mto wa Ruvu unaonywesha jiji la Dar chanzo chake ni Matombo.

Mlima wa Pangawe a.k.a Ng'alo





 Mlima wa Pangawe a.k.a Ng'alo njia ya kwenda Matombo ni mlima mkali una makona machache lakini hatari. Nilipokuwa mdogo nikisafiri na mama na bibi zangu walikuwa wanauogopa sana. Gari lilipokuwa likipanda au kushuka mlima huo wote walikaa kimya kabisa na wengine wakisali. Siku hizi mlima huo umechongwa na kuwekwa lami nyepesi.


Kanisa Katoliki- Mt. Patrick Morogoro

Hili ndilo Kanisa la Mt. Patrick lililoko Morogoro mjini, karibu kabisa na Hospitali ya Mkoa

Hapa ni Chalinze

Huu ni msimu wa mananasi. Angalia jinsi yalivyorundikana. Check pia vijana wanavyotembeza biashara kwa wasafiri. Usipoangalia kwa haraka unaweza kununua bidhaa duni na kwa bei ya juu.

Tusisahau kusoma mabango

Unapofika Kibaha ukitokea Dar umbali wa sehemu unakotaka kwenda zinasomeka hivyo.

Wakati nikielekea Morogoro

Traffic police huyu alikuwa kwenye kazi nzito ya kuongoza magari pale Ubungo

The Banzis walikuwa Matombo kwa Xmass

Linus Banzi (kushoto) na Renatus Banzi - wadogo zangu hawa machachari  ambao wengine wanawaita the twins (lakini si mapacha) niliwakuta Matombo wakila Xmass. Hapa wapo nyumbani kwa uncle Nestory Daulinge

The peace of mind


Jamani nauza nyumba 'yangu!'


A real relationship!


Wambagala tunavyotaniwa

Zamani walikuwa wanatutania kuhusu tunavyogombea mabus sasa wamekuja huku. Tuacheni na Mbagala yetu na nyinyi na Sinza Kijiweni yenu 'period.'

Anaweza kumpiga hata mbwa


How to burn fat

Kupunguza mafuta huyu kaamua kukoka moto kabisaaaa! Kimeeleweka kweli?

Habari ndiyo hiyo

Atajifunza tu kukwea mnazi hata kama bado anatambaa. House Girl anaweza kuchukua uamuzi kama huu na kisha kuondoka.

Don't worry about tomorrow!


Smartphone inauwezo wa kutoa picha jinsi utakavyo

Na ndivyo binti huyu alivyoitengeneza picha yake kutoka umbo flat na kuwa na umbo lenye wowowo balaaa!

Mtoto anaweza kuanikwa kama nguo

Ukimchezea 'house girl' naye anaweza kukuchezea zaidi. Usishangae kukuta mtoto wako ameanikwa kama nguo!

Hata 'house gir'l wa porini naye anajua kutesa