Monday, August 31, 2015

Familia inapowapa "company"

Waafrika tuna mapenzi makubwa. Tulipotembelea Afrika ya Kusini, dereva wetu pamoja na familia yake (mke na mtoto pichani- wengine ni wa Tz Dr. Nkuba na Bw. Mjema) walisafiri nasi na kutuelekeza kila tulichotaka kuelewa wakati wa safari hiyo. Binti huyo mdogo anaitwa Nashera.. kuna wakati aliponiona nakuja akaongea kwa Kiswati .....'mkulu' akiwa na maana mkubwa au mzee anakuja  alifurahi kwamba sasa safari itaanza kuendelea kama kawaida kwani mkulu ameshaingia ndani ya gari. Hata kwa Kiliguru 'mkulu' ina maana ni mkubwa kweli Waafrika wengi ni Wabantu!

No comments: