Monday, February 21, 2011

Gongolamboto ni zaidi ya Mbagala



Ndiyo ilivyokuwa usikuwa wa jumatano ya tarehe 16/2/2011. Ilianza kama nguromo za radi huku wengi tukitegemea mvua kubwa kunyesha hivyo kuondokana na mgao wa umeme! Haikuwa hivyo, kumbe ni mlipuko wa mabomu ulioacha simanzi kubwa kwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam. Kila mmoja aliokoa uhai wake. Wachache walikumbuka wake zao, watoto wao, mama zao, waume zao dada zao, kaka zao, shangazi zao, wajumbe zao na marafiki zao. Kuna walioacha magari, tv,dvd players, nyumba bila kufungwa na kuanza kukimbia hovyo. Kweli mabomu ya Gongo la Mboto ni zaidi ya Mbagala!

No comments: