Thursday, February 3, 2011

Watafiti wajengewa uwezo


Moja ya majukumu makuu ya Idara ya Utafiti na Maendeleo ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ni kujenga uwezo wa watafiti wake. Mwezi Desemba 2010, Idara iliandaa mafunzo ya wiki moja ili kuwanoa watafiti katika kufanya Impact na Adoption Studies ili kuweza kupima mafao ya teknolojia katika kukuza kilimo chetu na kupima jinsi wakulima walivyoweza kupokea teknolojia zilizozalishwa. Mafunzo hayo yalifanyika mjini Dodoma kwa kutumia wataalamu wa ndani wakiwemo Dr. January Mafuru (ARI-Ukiriguru), Dr Jackson Nkuba (ARI-Maruku) na Bw Deogratias Lwezaura (DRD-HQ-DSM). Mratibu wa Mafunzo Bw. Ninatubu Lema - Mkurugenzi Msaidizi - FSR/SE. Watafiti wapatao 30 walishiriki mafunzo hayo wengi wao wakiwa ni Wachumi Kilimo.

No comments: