Tuesday, November 24, 2009

Falsafa ya 'Zee la Nyeti'

Kama anaandika lugha ya kihuni, kama vile mtoto wa mijini. Lakini ndivyo mwandishi Henry Mdimu (Zee la Nyeti) anavyofikisha ujumbe wake kwa jamii kupitia gazeti la Mwananchi kila Jumamosi katika kurasa za starehe.

Blog hii imevutiwa sana na makala hizo na leo imebidi kuwafahamisha wasomaji wake ni vizuri ukalipata gazeti la Mwananchi la kila Jumamosi uweze kusoma falsafa ya Zee la Nyeti. Makala za Mdimu zina ujumbe mzito hasa kwa vijana. Lugha anayoitumia kufikisha ujumbe ni ile wanayoitumia vijana kwa hiyo haichoshi. Kwa mfano Jumamosi iliyopita kulikwa na kichwa cha habari kinachosmea 'Ngoma haipigwi kwa nyundo'.....hivi watu mkisikia mdundo wa ngoma mnafikiri ngoma huwa inapigwa kwa nyundo? Vijifimbo viwili tu, au samtaimz mkono wako tu...

Tarehe 31/10/2009. Mdimu alishuka na makala inayosema 'Ukiona manyoya...ujue keshaliwa' simulizi iliendelea hivi.....alipoingia tu anakutana na viata vya jmaa, saa iko mezani na kama nguo anazozijua hivi?.....ukiona unyayo si unajua kabisa kama kuna mtu kapita? .......Maana afadhali uone unyayo kuna siku utakuta manyoya, na itabidi ukubali...kwamba kuku keshaliwa.

Big Up Henry Blog hii imezikubali makala zako.

No comments: