Tuesday, November 3, 2009

JK amepania kuinua utafiti nchini


Gazeti la Habari leo la tarehe 2 Novemba 2009 limeandika kuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kutoa Tzs milioni 40 kwa ajili ya utafiti wa tufaa (apples) katika kituo cha Utafiti Uyole, Mbeya.

Ni hivi karibuni nimekuwa nikijiuliza kuwa kwanini biashara ya tufaa inaongezeka katika miji yetu wakati sioni wakulima wanaozalisha matunda haya hapa nchini. Jibu ni kwamba tofaa huagizwa kutoka Afrika ya Kusini.

Tanzania zipo sehemu ambazo tofaa zinaweza kuzalishwa kutokana na hali ya hewa ya maeneo hayo sehemu kama vile Lushoto (Tanga), Mgeta (Morogoro) na Mbeya. Iwapo utafiti wa kina utafanyika na kuweza kupata mbegu zinazoweza kustawishwa katika sehemu hizo kutakuwa hakuna sababu tena ya kuagiza tufaa kutoka nje ya nchi, kwahiyo auamuzi wa Mhe. Rais kutoa fedha hizo za utafiti ni chanzo cha kuanza kuzalisha tufaa bora hapa nchini.

No comments: