Tuesday, November 3, 2009

Tunapoteza shilingi milioni 28 za wakulima kama mchezo


Nimesikitishwa kusoma habari iliyoandikwa kwenye gazeti la Mtanzania la tarehe 2/11/2009 kuwa kiwanda cha sukari cha Ilovo kilichopo Kilombero kimetelekeza miwa ya wanachama 27 wa Chama cha Wakulima wa Miwa katika bonde la Kiliombero yenye thamanin ya shilingi ya Tanzania milioni 28. Habari hii imenistua kwa kweli, kwa umaskini walionao wakulima wetu kupoteza kiasi hicho cha fedha si jambo dogo hata kidogo. Si fahamu ni sababu zipi zilizopelekea uongozi wa kiwanda hicho kukataa miwa hiyo.

No comments: