Tuesday, November 24, 2009

Maalim Seif na Karume kukubaliana kuachana na uhasama ni uamuzi wa kihistoria

Jambo la msingi katika maisha ni kuondoa tofauti inayoleta misuguano katika jamii inayosababisha kudumaa kwa maendeleo. Msuguano uliokuwepo kati ya vyama vikuu vya siasa visiwani Zanzibar (CCM na CUF) umeleta athari kubwa katika jamii. Baya zaidi watu wamepoteza uhai kwa msuguano huu tena raia wa kawaida kabisa huku wakiwaacha viongozi wakuu wa vyama wakidunda!

Kitendo cha viongozi wa vyama hivyo huko Zanzibar kukubaliana kuachana na uhasama na kuijenga Zanzibar ni kitendo cha AFYA. Nawapongeza sana.

No comments: