Friday, October 23, 2015

Mimi Kipaumbele changu ni Kilimo

Hivi bila shibe utasoma? Kwanza chakula, Elimu baadaye. Nakumbuka nilipokuwa Tosamaganga High School    (Kidato cha  5-6) Mkuu wa Shule Mpogole alikuwa anatupatia chakula kizuri. Kila siku mchana sisi tulikuwa tunakula wali na nyama, mara moja kwa juma tunapata karanga za kukaanga (nusu kilo). Kweli tulikuwa na upungufu wa waalimu wa Chemistry na Biology lakini tulifundishana wenyewe kwa wenyewe hadi tulipopata walimu hao tukiwa kidato cha sita. Ajabu tulifaulu wote na sasa wengine ni maprofesa vyuo vikuu na wengine ni mabingwa katika fani mbalimbali kwa sababu tulishiba na si kushiba tu tulipata balanced diet. Muulize George Nyaupumbwe a.k.a Ngi wa TRA.

No comments: