Friday, October 23, 2015

Unapokuwa na watoto unajifunza lugha kwa wepesi zaidi

Nilipokuwa katika mji wa Tashkent huko Uzbekstan ambako nilipangiwa  kujifunza lugha ya Kirusi kabla ya kuendelea na masomo yangu ya uchumi kilimo, niliweza kujifunza lugha hiyo kwa kuongea kuongea na wananchi wa aina mbalimbali ili kupata uzoefu. Pichani niko na mwanafunzi mwenzangu kutoka Kigoma, Tanzania (jina nimelisahau) tukiwa na wanafunzi wa shule ya msingi. Tuliwaomba kupiga picha wakati wakirudi nyumbani kwao wakitoka shuleni. Tuliweza kuzungumza nao kwa kirusi na kutuelewa. Wakati huo tulikuwa tumetimiza miezi mitatu tu tangu tutoke nyumbani Tanzania mwaka 1987.(Picha kutoka Maktaba ya John Banzi)

No comments: