Monday, December 28, 2015

Bw na Bibi Michael Luanda miaka 30 ya ndoa


Hongereni Bw. na Bibi Michael Luanda wa Mbezi Msakuzi kwa kutimiza miaka 30 ya ndoa yenu. Michael Luanda ni rafiki yangu na ndugu yangu. Tunatoka wote Matombo, Morogoro tumesoma wote shule ya msingi Matombo. Sekondari Njombe tulikuwa sote kuanzia kidato cha kwanza hadi cha Nne. Wazazi wetu (wote marehemu) walikuwa wanafahamiana toka udogo wao na wote wameishi jijini Dar. Michael ndiye baba wa ubatizo wa mwanangu Sisty Banzi na Mama Luanda ni mama wa ubatizo wa binti yangu Catherine Banzi. Ni udugu wa familia na kiroho pia.

No comments: