Monday, January 22, 2007

BENKI KUU SARAFU CHAKAVU NI KERO

Jana Jumapili nilisafiri kwenda Mikocheni kwa basi la daladala. Nilipkuwa narudi nyumbani kwangu nilipanda basi la Kawe-Mtoni Mtongani. Nauli ni Tshs 250/- nilipotoa fedha hizo kondakta aking'aka, mzee hiyo hizo shilingi 50 chukua mwenyewe imechakaa hata kusomeka haisomeki. Mimi nilikuwa sikuiangalia sawasawa. Niliporudishiwa nikagundua kuwa kweli ilikuwa imesuguliwa sehemu ya wale swala na picha ya Mwl.Nyerere lakini bado ilikuwa inasomeka shilingi 50. Nikamwambia sina hela nyingine kama hutaki shauri yako. Dereva akazima gari akatoka kwenye kiti chake kuja kugombana na mimi. Nilijaribu kuwaelimisha lakini waliikataa sarafu ile hadi nilipotoa fedha nyingine. Ndani ya basi kuna abiria walioniunga mkono na kuna walionibeza kuniona kama msumbufu!
Sarafu hizi zinazoonyesha kuchakaa kwa kweli ni nyingi na zinaleta usumbufu mkubwa hasa kwenye usafiri na hata unapotaka kununua vitu ambavyo si vya gharama kubwa. Mtu akishaiona tu anasema mimi sipokei hiyo sarafu.

Lakini tukumbuke kuwa sarafu hizo ziko kwenye mzunguko na siyo senti ni shilingi. Je kukiwa na sarafu za thamani ya shilingi 50 milioni 10 ni kiasi gani cha fedha ambacho watu wanasema si fedha wakati bado ziko kwenye mzunguko? Milioni 500 ni shule ngapi za msingi zingejengwa? BENKI KUU SARAFU CHAKAVU NI KERO ZIONDOENI KWENYE MZUNGUKO.

No comments: