Monday, January 29, 2007

TUNATAKIWA KUFIKIRI KIDOGO TU

Tunatakiwa kufikiri kidogo tu ili kuweza kupunguza au kuondoa kabisa msongamano wa magari njia ya Kilwa. Nafahamu kuwa barabara ya Kilwa iko kwenye mpango wa kupanuliwa na kuifanya ya kisasa zaidi. Tuliahidiwa kuwa shughuli hiyo ingeenza mwezi Desemba 2006, lakini hadi hivi sasa, hali ni ile ile.

Huku tukisubiri kutengenezwa kwa mpango huu. Watumiaji wa barabara hiyo tufikiri kidogo tu. Hivi mashimo yaliyoko kwenye barabara hiyo yangezibwa vizuri tu hali ingekuwaje. Mashimo ya pale kwa Aziz Ally, Uwanja wa Sabasaba na pale Kurasini Mivinjeni yanakera sana na ni moja ya sababu ya msongamano barabara ya Kilwa. Kama kituo cha Mtoni Mtongani kingepanuliwa au kufanyiwa marekebisho msongamano usingekuwepo. Iwapo Halmashauri ya Temeke ingetengeneza ile barabara inayoanzia daraja la Tazara kwenda Tandika, kusingekuwa na sababu ya magari yanayoishia Tandika na hata yanayokwenda Buguruni, kupitia kwa Aziz Ally, msongamano ungepungua sana. Utaratibu mwingine ni kuyapangia magari ya mizigo muda tofauti. Ningependekeza yaanze shughuli zake kuanzia saa 3.00 asubuhi. Hivi sasa hakuna utaratibu maalum. Utakuta lori la mchanga, mkaa, magogo, tanker la mafuta, vipanya,"magobori" (DCM), Coaster, Suzuki, Pikipiki, baiskeli na waenda kwa miguu - barabara ni hiyo hiyo moja kweli patokosa msongamano hapo? Patakosa ajali hapo? Tunatakiwa tufikiri kidogo tu.

1 comment:

Unknown said...

leo nakusalimu tu.nimetembelea hapa kwa mara ya kwanza.