Tuesday, January 9, 2007

WATOTO WANAMATUMAINI YA MWAKA MPYA

Mwaka mpya huo.

Wengine mwaka mpya ndo mwanzo wa matatizo. Watoto wanataka kwenda shule, mfukoni kumekauka. Lakini kibaya zaidi kuna wengine waliozaliwa tarehe 1/1/ wanatakiwa kufanyiwa "birthday party". Usiniulize, mimi sikufanyiwa. Ila watoto wangu inabidi kuwafanyia.

Watoto wanamatumaini mapya. Kila mwaka mpya kwao ni mwanga mpya. Lakini wanatutegemea sana sisi wazazi wao kuwatayarishia njia. Watoto wetu wana matumaini ya kuishi maisha bora kuliko sisi. Hii inawezekana iwapo tutabadilika katika nyanja zote. Kikubwa turudishe maadili mema. Tuwalee watoto wetu kwa kufuata misingi ya dini na elimu dunia. Dini zote zinafundisha Upendo, Imani, Amani na Kusaidiana na Kusameheana.
Watoto hawa (pichani) kutoka kushoto Maggie Julius na Maria Mwaka Banzi wanafurahia mwaka mpya 2007.

HERI YA MWAKA MPYA

No comments: