Wednesday, March 23, 2011

Kisemvule Sports hoi kwa Wakali Kwanza

Timu chipukizi ya Wakali Kwanza kutoka Kisemvule imeiadhabu timu kongwe ya kijijini hapo Kisemvule Sports Club kwa magoli 2-0 kwenye fainali ya 'KISEMVULE CUP' iliyochezwa kwenye kiwanja cha Kisemvule Magengeni siku ya Jumapili tarehe 20/03/2011. Kwa ushindi huo washindi wamejinyakulia jezi na kikombe cha mashindano hayo. Nayo timu ya Kisemvule Kids Soccer Club imeibuka mshindi wa tatu na kukabidhiwa zawadi ya mpira mmoja.

No comments: