Wednesday, March 23, 2011

Ubunifu unatakiwa kukabili tatizo la Mbagala

Kwa kipindi hiki ambacho mvua nyingi zimeanza kunyesha,kero kubwa imeibuka kwa watumiaji wa barabara ya Kilwa kutoka Zakhem hadi Mbagala Rangi Tatu. Kipande hicho cha barabara kimeharibika sana. Hakuna maelezo sahihi yaliyokwishatolewa ili wananchi wafahamu kwanini kipande hicho hakikarabatiwi. Ubunifu mdogo tu wa kunyonya maji,kuchonga barabara na kisha kufukia mashimo kwa kifusi kikali hata kama hakuna lami ingesaidia kutatua tatizo.

No comments: