Wednesday, March 23, 2011

Tangazo la kudhalilisha mweusi

Kama umewahi kubahatika kusafiri na Shirika la Ndege la Afrika ya Kusini (SAA). Kabla ya ndege kuruka huwa linatolewa tangazo kupitia video clip linalowaeleza abiria jinsi ya kufunga mikanda, kuweka mizigo midogo kwenye cabin na mambo mengine. Kinachonishangaza ni ile sehemu inayoonyesha abiria mweusi asiye mwangalifu aliyekurupuka na kuweka mizigo kwenye cabin na kisha kumporomokea abiria mzungu (mweupe) na kumuumiza. Kwanini mzembe asiwe mzungu?

No comments: