Tuesday, May 20, 2008

DAR, ARUSHA, MBEYA-BADO

Mwezi Mei mwaka huu nimepata kuishi kwenye majiji yetu matatu ya hapa Tanzania:- Dar Es Salaam, Arusha na Mbeya. Ukweli ni kwamba pamoja na kuitwa majiji lakini viwango vyake bado ni vya chini ukilinganisha na majiji ya nchi nyingine nilizotembelea.

Kwanza majiji yote matatu ni machafu kwa mazingira. Karatasi zimezagaa hovyo, mitaro ya maji machafu, imeziba taka zimelundikana mitaani. Nilishangaa kuona hali hiyo ipo hata Arusha. Zamani Arusha ilikuwa ikisifika kwa usafi wake lakini sasa hakuna kitu. Arusha ina nuka! Ni shida kupata vyoo vya kujisadia ukiwa mjini itabidi uzunguke sana.

Na hapa Dar ndo kabisa balaa. Siku moja asubuhi nilikuwa nikisafiri kwenda Morogoro,wakati nilipokaribia kituo cha mabasi pale Ubungo nilikuta kinyesi cha mwanadamu kando ya barabara, aibu kabisa!

Mbeya nako, ushirikina hadi jijini. Asubhi na mapema, watu wanakwenda kazini pale airport -Mwanjelwa kichwa cha mbuzi kimewekwa kwenye makutano ya barabara! Jiji hilo!

Barabara za majiji yote hayo ni mbaya! Kwa mfano barabara nzuri pale Arusha pengine ni tatu tu nyingine hovyo kabisa. Mbeya 2 tu. Nyingine za mwaka 47. Hivi tuna mikakati gani na majiji yetu. Hivi kweli Watanzania tuko "serious" kwa hili? Aaa wahusika acheni uswahili angalieni majiji yetu yanavyoendeshwa aibu!

No comments: