Saturday, May 17, 2008

NAKUPA SHAVU MMILIKI WA MABUS YA SUMMRY

Hivi karibuni nilisafiri kwenda Mbeya kwa kutumia bus la Sumry. Kwa kweli huduma za mabus hayo ni nzuri kwa wakati tulionao sasa.

Kwanza wanajali muda. Pili mwendo si wa kasi tatu wahudumu wana lugha nzuri kwa wateja (wasafiri), nne mpango wao wa kutoa huduma ya vinywaji baridi na vichangamsha mdomo (pipi) vinakupa uhakika wa kutulia kwenye basi hata kama huna vijisenti vya kununulia chakula wakati ukisafiri. Isitoshe ukiwa ndani ya bus unapata muziki murua na picha za video.

Kwa hakika mabus ya Sumry yanafaa kwa usafiri kwa watu wa rika zote, watoto, vijana na wazee.Si shangai kuona kuwa sasa wamefunika kabisa kwa huduma za usafiri kanda za Nyanda za Juu Kusini (Mbeya, Rukwa, Iringa, Ruvuma).

Mara nyingi tumeona kampuni mbalimbali za usafiri zikianzishwa na kutoa huduma bab kubwa lakini baada ya muda huduma huzorota na kampuni hiyo kufa kabisa. Hebu tuangalie Scandavia inakoendea hivi sasa, choka mbaya! Sumry, isiwe ikawa "Mgema ukimsifia, tembo hulitia maji"

No comments: