Tuesday, May 20, 2008

MBAGALA HALI ILE ILE!

Mvua hizi za masika zinazokaribia kukatika zimewarudishia adha ya usafiri wakazi wa Mbagala ambayo walishaanza kusahau. Baada ya mvua kunyesha imeharibu sana barabara ya Kilwa hasa maeneo ya Mtongani hadi KTM na kuiacha katika mashimo makubwa wenywe wanayaita "mahandaki." Mashimo haya yanasababisha magari kupunguza mwendo na kuyakwepa mashimo hayo kutokana na hali hiyo kunakuwa na msongamano wa magari barabarani. Tatizo kubwa hapa kama nilivyokwisha eleza hapo juu ni mashimo.

Ninachojiuliza kuwa, Je, TANROADS wanasubiri mpaka mvua ikatike ndo waanze kukarabati barabara wakati watu wanateseka. Isitoshe wanapooanza kukarabati hurashia rashia tu ndiyo maana kila mvua inaponyeesha basi mashimo hutokea. Hii ndiyo hali halisi, si kweli kuwa Mbagala na vitongoji vyake ni vibaya na hazikaliki. Mbagala ni sehemu nzuri sana. Lakini barabara inawaangusha watu wa Mbagala. Kibaya zaidi kuna barabara moja tu ya kufika kati kati ya jiji.

No comments: