Friday, May 23, 2008

Tutafakari Mei Mosi




Kila mwaka ifikapo tarehe 1 Mei Wafanyakazi dunia nzima husherehekea sikukuu ya wafanyakazi. Kwa kulitambua hili Tanzania huwa inaadhimisha sikukuu ya wafanyakazi kwa maandamano, hotuba, michezo na maonyesho ya wafanyakazi. Sare za kutoka vyama mbalimbali vya wafanyakazi kama vile TUGHE, RAAWU havaliwa siku hiyo.




Nimekuwa nikijiuliza mara kwa mara hivi wafanyakazi huwa tunasherehekea nini ikiwa yale tunayohitaji mara nyingi huwa hayatimizwi, ahadi zinazotolewa huwa hazitimizwi.




Hivi kweli wafanyakazi huwa tunajipima kila mwaka kuwa tumetoa mchango gani katika ujenzi wa Taifa? Umetoa mchango gani katika maendeleo ya familia yako? Je, inakusaidia? watotot wa mjini wanasema inalipa? Inakuletea heshima na raha? Unajisikiaje unapoamka asubuhi na kwenda kazini. Unafahamu unachokwenda kufanya? Una ratiba ya kazi? Bosi wako na wafanyakazi wengine mnashirikianaje katika kukamilisha malengo?






Wengi hatujiulizi maswali hayo ya msingi, miaka nenda miaka rudi mambo ni yale yale tu. Wengi wetu tunafikiri Mei Mosi ni siku ya kupata sare kutoka vyama mbalimbali vya wafanyakazi.




Tutafakari MEI MOSI!

No comments: