Thursday, June 5, 2008

Inawezekana kuwapenda adui zetu ingawa ni vigumu

Tarehe 25 Mei mwaka huu, watoto watatu wa familia moja (ya Banzi) walipokea Ekaristi Takatifu kwa mara ya kwanza iliyotolewa na Balozi wa Baba Mtakatifu hapa nchini Kardinali Joseph huko Parokiani Vikindu, jimbo Kuu la Dar Es Salaam.

Watoto hao Peter L.J.Banzi, Catherine I.J.Banzi, na Sisty I.J.Banzi kutoka kijijini Kisemvule walikula mwili na damu ya Yesu Kristu baada ya kupata mafunzo ya muda wa miezi tisa kuhusu imani ya Kanisa Katoliki.

Katika mahubiri yake, Cardinali Joseph alisisitiza mapendo. Alisema kuwa inatupasa kupendana na kuwapenda hata maadui zetu ingawa ni vigumu lakini inawezekana

Mara baada ya kupata komunio, watoto hao walipokelewa kwa shangwe na ndugu na jamaa waliokuwa wakiwasubiri nyumbani kwao Kisemvule. Pamoja na mabo mengine waalikwa walisherehekea kwa chakula, vinywaji na burudani.

Katika wosia mfupi uliotolewa na baba yao mdogo Bw. Frederick Mloka, aliwaasa kufuata kwa ukamilifu mafundisho ya kanisa kwa sasa wamefungua njia ya kutambua kanisa na kulinda imani ya kanisa Katoliki.

Akitoa shukrani kwa ndugu na jamaa. Bw. Innocent J.Banzi ambaye ni Baba wa vijana hao aliwashukuru ndugu, marafiki, jamaa na majirani kwa ushirikiano wao walioutoa kwa hali na mali katika kufanikisha sherehe hiyo. Alisisitiza kupendana na kusaidiana wakati wote.

No comments: