Sunday, June 15, 2008

Bajeti-Mazoea?

Wiki moja baada ya kusomwa bajeti ya Taifa kwa mwaka wa fedha 2008/09 mambo ni yale yale, bia, soda bei juu. Vipaumbele ni vile vile- Elimu, Miundombinu, Afya, Kilimo......................

Watu wanazungumza sekta ya kilimo imesahaulika, kiasi kilichotengwa ni kidogo sana ukilinganisha na mchango wa sekta hiyo katika pato la Taifa na umuhimu wa Kilimo kwa wananchi wa Tanzania. Je, wanavuta kamba kwao? Sekta nyinngine wanasemaje. Tujenge viwanja vya Taifa kila mkoa!

Mimi ninajiuliza je, tunajifunza nini kutoka bajeti mbalimbali zilizopita? Kina nani wanaopanga bajeti? Nani wanaotoa maamuzi ya kupitisha bajeti? Je, kwa sasa ni akina nani wanaoichambua bajeti? Uelewa wetu kuhusu bajeti ni upi. Je, bajeti ni mazoea tuliyoyajenga au ni urithi kutoka kwa watawala wetu waliopita? (Wakoloni) bila kujiuliza maswali haya rahisi na kupata majibu, bajeti ni utamaduni wa kukaa bungeni kwa muda mrefu bila kutoka na maamuzi sahihi ya mipango ya nchi. Je wewe unasemaje?

No comments: