Sunday, June 15, 2008

Kutoka sare na Cameroun si mwujiza

Cameroon ni nchi iliyopo Afrika kama ilivyo Tanzania. Ni nchi ya dunia ya tatu. Nina maana uchumi wetu haupitani sana. Maendeleo yetu karibu ni sawa, tamaduni zetu ni sawa.

Tarehe 14/06/2008. Taifa stars ilitoka sare na Timu ya Taifa ya Cameroon " Indomitable Lions" katika kinyang'anyiro ya kupata tiketi ya kuwakilisha Afrika katika Kombe la dunia 2010 pamoja na lile la Mataifa huru ya Afrika.

Watanzania wengi hawakuamini kuwa Taifa Stars wanaweza kuibana Cameroon wasifurukute. Na wengi wanaamini kuwa Taifa Stars haiwezi kuifunga Camaroon. Huko ni kutojiamini, yote yawezekana iwapo tutajipanga sawa. Hata hivyo tusibweteke ni sare kwani hali yetu bado si nzuri point 2 tulizoweka kibindoni hadi sasa hazitoshi.

No comments: