Sunday, June 15, 2008

Maximo jifunze Kiswahili

Kocha mkuu wa mpira wa miguu hapa nchini Bw. Maxio Maximo ananishangaza sana eti hadi sasa hajui kuzungumza Kiswahili hata kile cha kubabaisha.

Maximo, ninavyofahamu mimi aliingia hapa nchini akiwa na kiingereza kibovu sana. Lakini amejiwekea mikakati ya kuhakikisha kuwa anakifahamu kiingereza vizuri. Kila anapofanyiwa mahojiano yeye hupenda kutumia kiingereza ambacho hakifahamu vizuri na hata hao wanaomuhoji hawakifahamu vizuri. Isitoshe TV au Radio zinazoendesha mahojiano naye zinatumia Kiswahili wateja wake wakubwa wanafahamu kiswahili. Ujumbe wa Maximo unamlenga nani?

Kama anataka kufanikiwa katika medani ya soka hapa Tanzania, inambidi aanze kujifunza Kiswahili kwa bidii zaidi ili aweze kuelewana na wachezaji, mashabiki na watanzania kwa ujumla. Vinginevyo muda wa kukaa Tanzania sikuzote utakuwa wa moto kwake!

No comments: