Sunday, June 15, 2008

Remote control inapofichwa na meneja

Jumamosi iliyopita nilitembelea Hotel moja iliyopo maeneo ya Magomeni jijini Dar Es Salaam. Ni hotel mpya ya hadhi ya kati.

Hotel hii inatoa huduma muhimu karibu zote kwa wageni wanaofikia kwenye hotel hiyo kwani hata huduma ya Internet inapatikana. Lakini cha kushangaza, watoa huduma kwenye hotel hiyo wanatoa huduma bila ya kujiamini.

Nilishangaa nilipokuta chumba kina TV lakini hakuna remote control. Nilipouliza nikapata jibu kuwa wateja huiba remote. Haya, remote inapopatikana, baadaya ya muda mrefu wa kuhangaika kupata stesheni nagundua kuwa hata waya wa Antena umenyofolewa! Ninapouliza inakuwaje? Jibu ni kwamba si kosa lao. Mwenye mamlaka hayupo! Ina maana mteja anapotoka antena na antena cable hukusanywa kuogopwa kuibiwa.

Hata baadhi ya maelezo muhimu ya jinsi huduma zinavyotolewa hotelini hapo ni shida kupatikana. Kwa kweli sielewi, remote inapofichwa na meneja!

No comments: