Thursday, June 26, 2008

Mabasi yaendayo kasi yanakuja kweli si uongo

Watanzania tunaogopa sana mabadiliko. Nikiwa ndani ya daladala nimenasa maongezi kati ya abiria na dereva. Dereva anasema tuone kama hayo mabasi yaendeayo kasi yatakuja, imeshindwa UDA! Abiria anasisitiza mabasi yatakuja na wajitayarishe kwa ushindani mkali katika sekta ya usafirishaji hasa jijini Dar. Nami nasema naam, hakuna kinachoshindikana, tujitayarishe kwa mabasi yaendayo kasi Dar. Sisi tunayasubiri kwa hamu. Wasiotaka mabadiliko kwa kulinda maslahi yao watambue hilo. Karibu sana mabasi yaendayo kasi hata kama mwaka 2o1o lakini yatakuja tu.

No comments: