Thursday, June 26, 2008

Precision Air kaza buti mwanangu

Nimewasili Tabora leo asubuhi kutoka Dar es Salaam kwa usafiri wa ndege wa Shirika la Precision Air. Nakwambia wamerudi kwenye chart mwanangu. Wako fit ile mbaya. Huduma zinazidi kuboreka si mchezo. Ukichelewa umeachwa. Wahudumu kauli safi. Viburudisho ndani ya ndege wawaa. Wameanza hata kutoa glass zao za Precision inapendeza eti jamani! Kaza buti Precision mwanangu mi nakupa shavu ile mbaya.

No comments: