Thursday, June 26, 2008

Muhogo unaweza kukutoa katika umasikini

Dkt. Nicholaus Mlingi wa TFNC anauona muhogo kama mkombozi wa mkulima na si zao la njaa kama lilinavyoonekana na wengi. Muhogo si zao la wakulima masikini. Muhogo unaweza kumtoa mkulima kutoka hali ya umasikini na kumpeleka kwenye hali ya neema kama atapata soko la uhakika, atatumia mbegu bora, ataongeza eneo la uzalishaji. Muhogo ni zao la biashara na chakula kwani lina matumizi mengi. Muhogo unaweza kutumika katika viwanda vya nguo (wanga), maabara ya kutengeneza madawa(asprin, syrup n.k.) viwanda vya kuokea biskuti na vyakula vya aina mbalimbali, viwanda vya uchapaji pia majani yake yanatumiwa kwa mboga (kisamvu).

Tatizo teknolojia nyingi hazijatumika kumsaidia mkulima kuweza kuzalisha muhogo kwa wingi na kuweza kumuingiza kipato na kuongeza pato la taifa. Mhandisi Mkuu wa Sayansi ya Chakula kwenye Taasisi ya Taifa ya Chakula na Lishe Bw. Felix Kimenya anabainisha. Anasisitiza kwa kusema kuwa sera ya kilimo iliyopo sasa inaipa muhogo kama nafasi ya zao la njaa.Tubadilike kisera na tuwezeshe wakulima wetu kwa teknolojia mbalimbali, kuwasaidia kuwapatia mikopo pamoja na kuwaunganisha wakulima katika vikundi vya uzalishaji wa zao la muhogo. Wenzetu wanatajirika kwa muhogo sisi bado tuko usingizini. mtazamo

No comments: