Thursday, June 26, 2008

HIVI KWELI KUNA MBUNGE WA KUKWAMISHA BAJETI YA SERIKALI?

Bunge linaloendelea hivi sasa ni la Bajeti. Imeshasomwa Bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi na Ofisi ya Waziri Mkuu. Majadiliano yamefanyika na yanaendelea kufanyika. Wabunge wanasimama na kutoa michango yao ile ile wanatoa kasoro zile zile za kila mwaka lakini hatimaye wanasema wanaunga mkono bajeti kwa asilimia mia moja. Mi mbona sielewi? Unaikosoa halafu unaiunga mkono kwa asilimia 100?

Leo asubuhi nikiwa uwanja wa ndege wa kimataifa pale Dar nilikutana na rafiki yangu wa siku nyingi mtaalamu wa Kodi Bw.Viani Komba ambaye tulisoma pamoja kule Tosamaganga Sekondari . Alisema, banzi hatuko serious na bajeti. Nchi nyingine wakati bajeti ya Wizara ya Fedha inasomwa siku hiyo ni ya mapumziko ya kitaifa kila mwananchi anafuatilia hatua hatua jinsi bajeti hiyo inavyowasilishwa na mwasilishaji baada ya kuwasilisha anapata glass ya maji hata kama nchi hiyo ni ya baridi! Hii ina maana bajeti ni kitu muhimu sana ni siyo cha mchezo kama inavyoonekana hapa kwetu. Lakini ninajiuliza kuna mbunge ambaye anaweza kukwamisha bajeti kama anaona ina kasoro?

No comments: