Thursday, July 3, 2008

Hebu soma filosofia hii ya Waluguru

  1. Bita ako si miyage (Kupita njia tofauti si vuzuri)
  2. Chikwili ng'awingagwa na seko ( "Chikwili" hafukuzwi kwa kicheko)
  3. Chibwarabwatzi ukaye, kumgunda hoya
  4. Chibweregeni dawalaga uye, mdawalo gumuhonza ng'uku ( "chibweregeni" ucheze ukumbuke kurudi nyumbani mchezo umemponza kuku)
  5. Chimbulumbulu kokwila mti gwagumanyile ("Chimbulumbulu" hupanda mti anaoufahamu)
  6. Chujile cho chako, chiliumoto chamuhimba kaburi (Ulichokula ndiyo riziki yako kinachopikwa ni cha mchmba kaburi)
  7. Chamunu mahvi ung'achona uchiteme mate ( Cha mtu ni mavi na ukikiona ukiteme mate)
  8. Chihvile chola (Kilichoiva kimeoza)
  9. Mguluko gwa ng'anga wosi lunga lumwe
  10. Mlonga yeka kahuma
  11. Mwana ng'weleke mkulu miyago (Mtoto usiyemzaa mkubwa mwenzio)
  12. Kala mwatzi uhone (Kaa uchi upone)
  13. Chilondola cha imchua chohonela tungwe (Kidonda cha masikini huponywa kwa umande)
  14. Msimulila mvula imtowela (Msimulia mvua imemnyeshea)
  15. Mgulu gwangile (Mguu uliotembea nao)
  16. Mbewa kengila mchikalango (Panya kaingia kwenye kikaango)
  17. Moko gwamile mahvi ng'ugukana (Mkono uliokamata mavi haukatwi)
  18. Chinyala chikoma ng'enge (Aibu imemua kenge)
  19. Msongola lwiko kalema ukulakala
  20. Mtowa malati inguhvu muda (Mpiga baragamu nguvu inatoka tumboni)
  21. Ukulu tzalala (ukubwa jalala)
  22. Tudawale hatwibone (Tucheze tunapoonana)
  23. Uchuwa we ng'anga, inguku kana mtwatza (Ukiwa wa kanga kuku ana mfadhili)
  24. Kulawile ichijo kwa nzala (kulikotoka chakula kuna njaa)
  25. Uje chikuleme (Ule kikukatae)
  26. Cha nzala chilola hasi (Chenye njaa kimeangalia chini)
  27. Isi igalamka indetsi kowinga yumbwa (Nchi imechangamka ndezi anafukuza mbwa)
  28. Legela wakohe (Legea wakufunge)
  29. Msegetsa mno katula imbugi
  30. Mbama usafi kajila hasi
  31. Chuhuwile yumbwa kaja
  32. Cheleko cheleko ne mwenye mwana (Cheleko kipigwe na mwenye mtoto pia)
  33. Udodo ng'uku
  34. Mabuku mengi ng'agohimba mshimo gugendegende (mapanya wengi hawawezi kuchimba shimo mrefu)
  35. Tzeketzeke ni jako (Hata kama mpumbavu ni wako)

Ongeza kama una zaidi ya haya

No comments: