Monday, July 28, 2008

Wagani wa kilimo wapatiwe vitendea kazi

Huwezi kumuona mhasibu asiye na calculator, daktari na kipima mwili chake, dereva na gari lake, mchoma mahindi na jiko lake, mama/baba ntilie na sufuria zake.
Utamtambuaje afisa ugani wa kilimo asiye na kitendea kazi? Anashauri wakulima wapande mazao kwa nafasi zinazokubalika huku kipimio hana. Anashauri wapande mbegu ya mahindi ya TMV 1 yeye mwenyewe haijui. Anawashauri wakulima wampunga watumie mbolea ya kukuzia aina ya UREA yeye mwenyewe wala hajui inakopatikana. Ndiyo maana mbunge mmoja alikumbusha kwa kweli, wakatia umefika sasa wa kuhakikisha kuwa maafisa wagani wa kilimo wanapewa vitendea kazi. Ndipo hapo tutakapowaona wakichacharika kweli kweli na watu wakiwathamini kama wanavyomthamini daktari.

No comments: