Wednesday, July 9, 2008

ARI -Tumbi-TABORA-Hazina ya Kilimo Misitu

Utafiti wa Kilimo nchini umegawanywa kwenye kanda saba nazo ni Kati, Mashariki, Ziwa, Kaskazini, Kusini, Nyanda za Juu Kusini na Magharibi.

Kituo cha Utafiti wa Kilimo Tumbi -Tabora (ARI-Tumbi) kanda ya Magharibi ndicho chenye jukumu la kushughulikia utafiti wa Kilimo Misitu (Agro Forestry).

Wengi wetu hatufahamu Kilimo Miti ni nini? Mtafiti wa Kilimo Misitu kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bw. N.Lema anaeleza kuwa watu wengi wanachanganya Kilimo Mseto (Mixed Farming ) na Kilimo Misitu (Agroforestry). Kilimo Misitu ni kilimo kinachohusu ustawishaji wa mimea kwa ajili ya kuni malisho ya wanyama, kurutubisha ardhi, ujenzi, matunda na mimea ya dawa.

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tumbi kwa muda mrefu imekuwa ikifanya utafiti wa Kilimo Misitu kwa kushirikiana na ICRAF. Utafiti umekwenda mbali zaidi hadi kubaini miti ya matunda pori na dawa na aina mbalimbali za miti imeshakusanywa ndani na nje ya Tanzania.

No comments: