Friday, July 11, 2008

Hakika tunaweza kutumia umeme wa jua

Juzi niliona picha moja nzuri kwenye gazeti la kila siku la Kiingereza "DAILY NEWS" yenye maelezo - Wavietnam wakushughulikia kuweka Panel za Solar kwa ajili ya umeme vijijini.
Niliisoma makala ile kwa makini sana. Nilichogundua ni kwamba tayari Wavietnam wameshaona umuhimu na uwezekano wa kutumia umeme wa mionzi ya jua ili kutoa nishati huko vijijini hata kwa kuanzia kutoa mwanga tu.

Jumapili iliyopita katika pitapita yangu pale Kariakoo karibu kabisa na mzunguko wa barabara ya Uhuru na Msimbazi niliona duka moja linauza vifaa vya umeme wa jua. Nilipouliza niliambiwa vinauzwa kwa jumla ya shilingi 225,000/= na vinaweza kuwasha umeme wa taa nne ndogo. Kumbe inawezekana!

Inawezekana umeme huu ukaanza kasambazwa vijijini hata kwa njia ya mkopo. Laki 2 ni sawa na kuuza magunia 4 ya mpunga. je haiwezekani kufunga "solar" kwa wakulima wa mpunga, kahawa, chai, mahindi, maharage, ndizi, viazi. Tatizo hatuna mkakati na hatutaki kusoma wataalamu wetu wanashauri nini kuhusu nishati. Kwa kifupi watu ni wabinafsi na hatutaki kuwasaidia wenzetu walioko vijijini.

Tuanze sasa kutumia umeme wa jua. Uwezekano upo na ni rahisi. Vinginevyo tutasoma asilimia 90 ya Wavietnam sasa wanapata umeme. Wameshatupita kwenye kilimo na viwanda sasa wanaangalia mambo ya nishati. Sisi tunabaki kusema aah! Wote tulikuwa masikini miaka ya sabini. Haisaidii kitu.

No comments: