Wednesday, July 9, 2008

Bado sijamuona mfungaji Taifa Stars

Mimi sijui kama tunaye mfungaji wa kuaminika kwenye timu yetu ya Taifa Stars. Magoli yote yanayopatikana yanapatikana kwa bahati tu. Leo kafunga Abdi Kassim, kesho Emmanuel Gabriel, kesho kutwa Danny Mrwanda. Kwa hakika hatuna mfungaji!

Miaka ya sabini hadi tisini tulikuwa na wafungaji wakuaminika kama akina Edward Chumila (Marehemu), Abdallah Kibaden, Gibson Sembuli (Marehemu), Kitwana Manara Popat, Jumanne Masumenti (Marehemu), Peter Tino, Zamoyoni Mogella, Mohamed Salim na wengineo wengi. Hata wakishika mpira unategemea goli litapatikana. Walijua kujipanga vizuri ili wapate goli. Wakati kona inapigwa ilikuwa ni lazima umchunge sana Kitwana Popat Manara au Jumanne Masumenti na walijua kufunga kwa kichwa, mpira unaweza kudunda chini kwanza kabla ya kuingia au kuupeleka pembeni kabisa mwa goli.

Siku hizi hata tukipata kona 10 ni bure. Wachezaji wetu wa mbele si watafutaji wa magoli. Hivi kweli hatuwezi kuwapata wafungaji wazuri wa magoli kama ilivyokuwa zamani? Bila ya kufanya hivyo hakuna maajabu.

No comments: