Tuesday, July 29, 2008

Shughuli imeanza Mtongani-Mbagala

Makaravati yanazikwa ardhini, njia za mkato zinatengenezwa, nguzo mpya za umeme zinasimikwa. Kweli, awamu ya Pili ya ujenzi wa barabara ya Kilwa imeshaanza na mambo yanakwenda kwa kasi ya ajabu. Siku hizi kutoka kwa Aziz Ally hadi Mtongani ni kuteleza tu. Imebaki sehemu ndogo pale Mtoni Mtongani. Wananchi wanangojea maajabu wayaone ya kupitisha barabara pale darajani itakuwaje? Twasubiri tuwaone Kajima.

No comments: