Friday, July 11, 2008

"Conductor Perhaps!"

Leo asubuhi wakati nakuja kazini kwenye bus nililopanda nilimkuta "conductor perhaps" mmoja. Kwanini nasema hivyo. Kondakta huyo alikuwa wa ajabu kweli lugha chafu ya matusi, amevaa hovyo hovyo tu. Nina maana hana vazi rasmi. Lakini alionekana kama mpiga debe tu huku akiwa amening'inia mlangoni kazi yake ni kutoa amri-Eeeh mwanangu rudi nyuma! Alifoka.Hiyo ndiyo ilikuwa kazi yake na maneno machafu kwa abiria.

Abiria wa bus lile nami nikiwa mmoja wapo hatukuweza kumvumilia hata kidogo. Tukaanza kumuelimisha.
  • Kwanza kijana hatukutambui
  • Huna vazi rasmi
  • Hakuna kazi unayoifanya hapo mlangoni
  • Lugha yako ya matusi inatukera

Tunachoweza kukifanya ni kukuwasilisha kwa Kamanda Kova akushughulikie.

Baada ya kupashwa nafikiri alitambua makosa yake na aliufyata. Huyo ndiye "Conductor Perhaps."

No comments: