Thursday, July 24, 2008

Tuwatambue wakulima wetu

Sawa kabisa, inavyoelekea, bado hatujawatambua wakulima wetu. Ni kina nani? wangapi? wako wapi? na wanahitaji nini?wanafanya nini kwa sasa? wanafanyaje? kwanini wanafanya hivyo? Hayo ni maswali ya msingi kabisa yanayotakiwa kufahamika kutoka kwa wakulima wetu ili tuweze kuwatambua.

Tusipowatambua, mipango ya kuwapatia pembejeo za kilimo itakuwa ni ya mashaka, mipango ya kuwatafutia masoko utakuwa ni wa kubuni tu, teknolojia za kilimo zinazobuniwa kumsaidia mkulima katika kuboresha uzalishaji zitakuwa ni za watafiti tu ni si mahitaji ya mkulima, tunaweza kununua matrekta na kuyasambaza kila mkoa kumbe si kila mkoa unahitaji matrekta idadi sawa, tunaweza kumwaga mabilioni kwa kutoa mikopo kwa wakulima kumbe wakulima hawajui jinsi ya kutumia mikopo hiyo na pengine mikopo inaweza kutolewa wakati usio mwafaka kwa kilimo.

Kwahiyo basi suala la kuwatambua wakulima wetu ni la msingi kama baadhi ya wabunge walivyochangia kwenye hotuba ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika mwaka 2008/09

No comments: