Monday, July 28, 2008

Tuwe tayari kutoa - Asema Padri Ngowi

Padri Ngowi wa Parokia ya Mkuranga amewaasa waumini wa Parokia ya Vikindu jimbo Kuu la Dar Es Salaam kuwa wawe wepesi na tayari kutoa kuliko kupokea. Padri Ngowi aliyasema hayo katika mahubiri yake aliyoyatoa Jumapili ya tarehe 27 Parokiani hapo.

Alisikitika kwa kusema kuwa, waumini Wakatoliki wamezoweshwa kupewa kuliko kutoa. Wakati umefika sasa wakuendesha Kanisa wenyewe bila ya kuwategemea wazungu na wamisionari wa kigeni. Watawa wanatakiwa kupata mahitaji muhimu kama vile chakula, mavazi, malazi na usafiri ili weze kutimiza wajibu wao wa kutoa huduma ya kiroho. Kwa hiyo ni wajibu wa waamuni kutoa sadaka na kulipa zaka kama inavyotakiwa na kanisa.

Akihubiri bila kuchoka, huku akirandaranda ndani ya kanisa na kuwahamisisha waumini na hatimaye kufanya harambee ya mavuno iliyoweza kukusanya zaidi ya shilingi 1,000,000 (fedha taslimu na ahadi) kwa ajili ya tegemeza parokia. Waumini walichangia kiwango cha sh 500/= hadi 150,000/=

No comments: