Wednesday, July 9, 2008

Fursa ipo kwenye Kilimo Misitu

Timu ya Kupelemba na Kutathmini shughuli za Utafiti Kanda ya Magharibi imebaini kuwa kuna fursa kubwa kwa wasomi asilia kuendeleza utafiti wa Kilimo Misitu hadi kufikia ngazi ya shahada za uzamili (MSc) na Uzamivu (PhD).

Fursa hii imebainika baada ya kuona kuwa kuna mazao asilia mengi kwenye mistu yetu ya asili ya miombo kanda ya Magharibi. Misitu hii ina toa matunda mengi ya asili ambayo yakifanyiwa utafiti yanaweza kutoa mazao mbalimbali ambayo yatasaidia kuchangia kipato cha familia kwa wakulima wetu.

Kinachotakiwa kwa sasa ni Serikali kuhakikisha kuwa programu hiyo inapata fedha za kutosha, usafiri wa kuaminika, na wataalamu ili iweze kuendeleza utafiti uliokwisha anzishwa na kuleta mafanikio lakini kutokana na ufinyu wa bajeti utafiti huo unaanza kurudi nyuma.

No comments: