Wednesday, July 9, 2008

Mtongani hadi Kariakoo sasa dakika 10

Ile adha, karaha na kashkash ya usafiri barabara ya Kilwa inatarajiwa kupungua kwa kiasi kikubwa baada ya mkandarasi wa Kampuni ya Kajima kukaribia kumaliza kujenga kipande cha barabara kutoka Bandarini hadi Mtoni Mtongani.

Jumapili iliyopita nilitumia dakika 8 kutoka Mtongani hadi Kariakoo. Sehemu kubwa ya barabara imeshakamilika kilichobaki ni nakshi nakshi pamoja na kipande kidogo unapokaribia Mtongani penyewe. Mkeka umeshamwagwa kwa sehemu kubwa ya barabara.

Dalili za kuanza awamu ya pili zimeanza kuonekana. Tayari pale Mbagala Zakhem kambi ya ujenzi inajengwa na sehemu kubwa imeshaanza kusafishwa.Tusubiri na tuone adha ya usafiri Mbagala itakuwa historia, wawekezaji karibuni Mbagala na Vikindu!

No comments: