Monday, July 28, 2008

Mafuta si leo, lakini hili la chakula tunaweza sasa


Hatujui ni lini Tanzania tunaweza kuzalisha mafuta mengi na kuweza kujitosheleza kwa matumizi ya ndani na kuuza ziada. Lakini kwa chakula tunaweza hata mwaka huu tukijipanga sawasawa. Hili linawezekana iwapo mipango yetu itawekwa kwa kuweka kipaumbele katika uzalishaji wa chakula. Tanzania tunayo fursa kubwa zaidi katika kilimo. Tuna ardhi ya kutosha, tuna maji ya kutosha, wataalamu wa kutosha na wananchi wetu asilimia 80 wanategemea kilimo hivi kweli hili nalo hatulioni? Tunataka tuletewe programu ya kuzalisha chakula kutoka World Bank? Hakika hili la kuzalisha chakula tunaweza sasa.

No comments: