Monday, July 28, 2008

Kwa hili la kuiogopa Simba, Yanga hawana la kusingizia

Kitendo cha Klabu Bingwa ya Soka ya Tanzania kwa mwaka 2008 - Dar Young Africans kushindwa kufika uwanjani kupambana na watani wao wa jadi Simba Sports Club ya Dar Es laam siku ya Jumapili katika pambano la kumpata mshindi wa tatu wa kombe la Kagame limeitia doa kubwa timu hiyo, Dar Es Salaam na Tanzania nzima.

Sababu za madai ya malipo ya ziada hayana msingi. Yanga kanuni za mashindano hayo wanayafahamu, iweje leo kusisitiza walipwe fedha zaidi kuliko hata anachapata mshindi wa mashindano hayo, ni kichekesho!

Dar Young Africans wamefanya usajili mzuri na wa gharama mwaka huu, wanamakocha watatu wakigeni tena wazungu! Hata golikipa mzungu pia amesajiliwa yanga, iweje leo kukacha mechi hiyo? Mi sielewi, hata Nicholaus Musonye ameshindwa kuwaelewa Yanga na hata kuwaita "wahaini wa CECAFA." Tusubiri maamuzi ya CECAFA kwa tukio hilo.

No comments: