Thursday, July 24, 2008

"Mapinduzi ni Vita"

Mara nyingi neno Mapinduzi hutumiwa sana na watu wengi wanapotaka kufanya mabadiliko ya kitu fulani au jambo fulani. Watu wanapoingia kwenye mapambano ya aina yoyote hawachelei kusema kuwa tuko vitani. Maneno haya ukiyaunganisha na "ni" unapata sentensi inayosema "Mapinduzi ni Vita."

Nimeshasikia mara nyingi kutoka kwa viongozi wetu hapa nchini kuwa tunataka kufanya mapinduzi katika kilimo. Je, wanafahamu kuwa mapinduzi ni vita? Ni nilazima kujiandaa barabara, kwenye vita hakuna kurudi nyuma hadi ushindi upatikane. Makamanda je wapo? Makomandoo wa kilimo wapo? Ni kina nani hao? Tusipotambua hilo mapinduzi ya kilimo ni ndoto.

No comments: