Thursday, July 24, 2008

Uhariri wa kursasa gazeti la Mwananchi ni wa wasiwasi

Kwa wale wasomaji wa magazeti ya kila siku, sijui kama mlipata bahati ya kusoma gazeti la Mwananchi la tarehe 13 Julai 2008. Gazeti hili lilikuwa na kasoro kadhaa katika upangaji wa kurasa za magazeti na hasa tarehe. Ukurasa wa 28 ulisomeka Juni, 22 na ukurasa wa 26 ulisomeka Juni 14, 2008. Lakini ukweli ni kwamba gazeti hilo lilikuwa ni la Jumapili tarehe 13 Julai 2008. Ndiyo maana nasema uhariri wa gazeti la mwananchi ni wa mashaka. Inaelekea ni tatizo la "cut and paste" ambao wasanifu wa kurasa hawakugundua, naomba muwe makini.

No comments: