Wednesday, July 9, 2008

Tunategemea kuvuna kutoka misitu ya asili

Sasa imebainika kuwa misitu yetu ya asili ni mali.
Hivi karibuni niliweza kuzungumza na baadhi ya watafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo-Tumbi, Tabora kuhusu utafiti wa Kilimo Misitu. Nilichojifunza ni kwamba misitu yetu ya asili ikitumiwa vizuri inaweza kabisa kuwasaidia wakulima wanaoishi karibu na misitu hiyo kuboresha maisha yao kwa mazao yanayotokana na misitu hiyo.

Misitu yetu kama ilivyo kwa vijiji vyetu ni vyanzo vya kuni lakini pia hutoa malisho ya mifugo yetu, hutoa mbao kwa ajili ya ujenzi na samani, hurutubisha ardhi, hutoa dawa na matunda pori ambayo yakitayarishwa yanaweza kutumika kwa kutengeneza mvinyo, jamu na pombe aina ya amarula.

Watafiti wa kituo hicho wameshaanza kufanya utafiti wa miti aina mbalimbali na baadhi ya teknolojia zimeshapelekwa kwa wakulima na kupokelewa vizuri. Hivyo tunategemea kuvuna kutoka kwenye misitu ya asili.

No comments: