Saturday, May 17, 2008

WANAWAKE - Wajasiriamali Arusha

Ukitaka kuona jinsi wanawake wanavyochacharika kutafuta maisha au kitu pesa basi nenda Arusha. Wanawake wa Arusha hawatulii. Biashara za mboga na matunda huko sokoni karibu asilimia 80 zinafanywa na wanawake. Leo asubhi nilikuwa nikipita pita kwenye baadhi ya mitaa ya Arusha nimewakuta wanawake wakiwa na malundo ya mitumba wamebeba kichwani na wengine wametandaza chini ni itumba ya kila aina. Soksi, mashati, suruali na makoti.

Pale kati kati ya mji sokoni, nilibahatika kununua sabuni nzuri sana ya mche ambayo inafaa kwa kufulia na kuogea (nafikiri zinatoka Kenya). Aliyeniuzia ni mwanamama tena kilema wa mguu.

Hawa ndo wanawake wa Arusha. Na usidhani unaweza kuwasumbua kwa "vijisenti" vyako kwani wanavyo tena viko hapahapa Tanzania! Hongera sana wanawake wa Arusha.

No comments: