Friday, January 30, 2015

Tukiwa Modiporum-India kwenye Taasisi ya Utafiti ya Mifumo ya Kilimo

Tulipokuwa kwenye ziara ya mafunzo nchini India mwaka 2014, timu yetu ilipata fursa ya kutembelea Taasisi ya Utafiti wa Mifumo ya Kilimo nchini India huko Modiporum. Hapa tulikutana na watafiti nguli wa Taasisi hiyo na kuongea nao jinsi wanavyoendesha utafiti wa aina hiyo ambapo hapa kwetu ni sehemu ndogo tu. Tulipata fursa ya kutembelea tafiti zinazoendelea hapo hapo kituoni zinazohusu mifumo ya kilimo. Baada ya hapo tulipata picha ya pamoja.Mwenye vazi la Kihindi ni Dr. Mohamed Bahari aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambaye alikuwa ndiye kiongozi wa msafara kutoka Tanzania.

No comments: