Monday, July 6, 2009

Kilimo cha Mpunga Kanda ya Kaskazini kinalipa

Kutokana na tafiti zilizofanywa hivi karibuni wataalamu wa uchumi jamii na mifumo ya kilimo wamebaini kuwa kwa eneo la hekta moja, kilimo cha mpunga kinalipa zaidi ya mahindi na mtama iwapo mkulima atatumia mbegu bora na pembejeo muhimu za kuzalisha mazao hayo ikiwemo mbolea. Imedhihirika kuwa kwa hekta moja mkulima anaweza kupata faida ya Tshs 1,412,100/= akilima mpunga wakati mahindi yanaweza kutoa faida ya Tshs 1,269,400 na mtama Tshs 163,200/= . Mahesabu haya yamefanywa kwa kuzingatia bei za mwaka 2006/07.

No comments: