Thursday, July 23, 2009

Nishati ya Jua gharama ziwe nafuu

Moja ya magazeti ya kila siku hapa nchini limeandika kuwa Serikali imepania katika kuhakikisha kuwa nishati ya Jua inapewa kipaumbele kinachostahili. Huu ni mtazamo mzuri. Jambo jema ni utekelezaji wake. Iwapo tutafanikiwa katika hili nina uhakika tutasonga mbele kimaendeleo kwa kasi zaidi. Upatikanaji wa jua hapa nchini si wa mashaka kama ilivyo kwa nchi za ulaya. Hii ndiyo sababu kubwa ya kuweka msisitizo wa uendelezaji wa nishati ya jua. Kwa hili mijini na vijijini watanufaika sana lakini endapo tu gharama za nishati hii zitakakuwa nafuu kwa wananchi wa vipato mabalimbali.

No comments: